Friday, May 3, 2013

WOSIA WA LADY JDEE ALIOUANDIKA KAMA IKITOKEA AMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA

Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.

Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.
Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.

Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria.
Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu.

Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia.
Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa, Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa.

Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao.
Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni.

Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu.

Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige wame
Enyi mtakaokuwa hai baada yangu.

Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai
Hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu.
Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia.

Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge.
Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka.

Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha, Hamuwezi kumiliki dunia..
Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star..

Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie??.
Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu.

Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili.
Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri.
Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani??
Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi??

Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili.

Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu.
Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma??
Roho gani hiyo??

Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu

JIDE

Monday, November 26, 2012

SHAROMILIONEA AFARIKI DUNIA


MSANII WA MAIGIZO NA MUIMBAJI WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA(BONG FLEVA),HUSSEIN MKIETY 'SHAROMILLIONEA (PICHANI) AMEPATA AJALI MBAYA MAENEO YA MUHEZA KATIKA KIJIJI CHA LUSANGA MKOANI TANGA AMBAPO NDIO NYUMBANI KWAO NA KUPELEKEA KUPOTEZA UHAI WAKE
KWA MUJIBU WA WASANII WENZAKE AMBAO NI MWANADADA SHILOLE NA STEVE NYERERE( KWA WAKATI TOFAUTI) WAMETHIBITISHA KUTOKEA KWA AJALI HIYO LEO JIONI

CHANZO CHA KUTOKEA KWA AJALI HIYO BADO HAKIJAJULIKANA

Saturday, November 24, 2012

MSANII WA FILAMU JOHN MAGANGA AFARIKI DUNIA

 RIP JOHN MAGANGA
Kwa mara nyingine tena wiki hii tasnia ya filamu imepoteza msanii mwingine baada tu ya kumaliza mazishi ya Mlopelo. Msanii John Maganga amefariki katika hospitali ya Muhimbili.  Taratibu za mazishi bado zinafanyika.

Ni hivi karibuni tu msanii huyu alisema kuwa amefungua Kampuni yake ijulikanayo kwa jina la Jom Entertainment Co. Ltd, pia akaeleza kuwa alianza kuona kipaji chake tangia mwaka 2001 alipokuwa akifundishwa na msanii nguli wa filamu nchini Ndumbago Misayo 'Thea' ambaye alikuwa mwalimu wake wa maigizo wakati wapo kanisani pale Mwananyamala, baada ya hapo filamu ya kwanza iliyokwenda kwa jina la Miracle of Love  ambayo ilifanya vizuri sana katika kumtambulisha kisanaa nchini. Mwaka 2008 alishauriwa na ndugu yake Deogratias Shija kufungua kampuni yake kwa ajili ya kuendeleza fani ya filamu, kazi ambazo ziko tayari ni Beautfuls aliyowashilikisha wasanii kama Aunt Ezekier, Haji Salumu 'MBoto' na wengine wengi
Mungu aiweke pema roho ya msanii huyu ambaye ameondoka wakati anaanza kuchipua.

Saturday, November 10, 2012

Barabara kuu (super highway) ya Nairobi kwenda Thika imefunguliwa rasmi jana na Rais Kibaki. Je, unahisi Bongo tutaweza kuwa na barabara kama hii? Kama ndiyo, lini?

Barabara kuu (super highway) ya Nairobi kwenda Thika imefunguliwa rasmi jana na Rais Kibaki. Je, unahisi Bongo tutaweza kuwa na barabara kama hii? Kama ndiyo, lini?

Thursday, November 1, 2012

UZINDUZI WA BARABARA YA MKUU ROMBO-TARAKEA.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea kabla ya kufungua rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na washika dau wa miundombinu wakikata utepe  ishara ya kufungua rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea  Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaidiwa na Mbunge wa Rombo Mhe Joseph Selasini kukunjua pazia kama ishara ya kufungua rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea leo Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Mbunge wa Rombo Mhe Joseph Selasini kukunjua pazia kama ishara ya kufungua rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia jambo na Mbunge wa Rombo Mhe Joseph Selasin katika hafla ya ufunguzi rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.

Friday, October 19, 2012

BREAKING NEWZZZ

jijini Dar es Salaam hali si shwari  maeneo ya Kariakoo maduka kadhaa yamefungwa kufuatia vurugu kama hizo baada ya Swala ya Ijumaa kufuatia pia kukamatwa kwa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania Sheikh Ponda yamekuwa ni matokeo ya vurugu watu kukimbizana huku Polisi wakidhibiti Usalama na Amani kuelekea harijojo.(Picha na Maktaba).

Maeneo ya Posta karibu na Wizara ya Mambo ya Ndani Askari wameweka utepe wa kudhibiti watu kuingia katika maeneo hayo kitendo kilichosababisha shughuli nyingi kusimama.

Pichani ni maeneo ya Kariakoo magari ya jeshi JWTZ zaidi ya 8 yakiwa katika doria  maeneo ya Kariakoo.

Sunday, October 14, 2012

QN.Write a program that will print the contents of an array typed by the user in either ascending or descending order depending on the user`s choice.

import java.util.Arrays;
import java.util.Collections;

public class Djshark{

public static void main(String args[]) {
String[] companies = { "Google", "Apple", "Sony" };

// sorting java array in ascending order

printNumbers(companies);
Arrays.sort(companies);
System.out.println("Sorted String Array in ascending order : ");
printNumbers(companies);

// sorting java array in descending order

printNumbers(companies);
Arrays.sort(companies, Collections.reverseOrder());
System.out.println("Sorted int Array in descending order : ");
printNumbers(companies);

}

public static void printNumbers(String[] companies) {
for (String company : companies) {
System.out.println(company);
}
}

}

Thursday, October 4, 2012

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) anatarajiwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika jiji la Arusha siku ya Jumamosi tarehe 06.10.2012 kuanzia saa 8 mchana. Pamoja na mambo mengine Kiongozi huyo wa CDM pia atatumia mkutano huo kuzindua rasmi kampeni za udiwani katika kata ya daraja mbili,uzinduzi huo utafanyika katika viwanja vilivyopo mtaa wa NDARVOI.

Tayari kuna hekaheka kubwa katika jiji la Arusha kuhusiana na mkutano huo ambapo mazungumzo ya watu mbalimbali yanazungumzia mkutano huo unaotarajiwa kuwa gumzo.

Taarifa za awali zinasema mkutano huo pia utatumika kufuta nyayo za chama cha CUF ambacho kilisomba watu Dar-es-Salaam kwenda kuwahutubia Arusha ili kuepuka aibu ya kukosa watu.Pia inadaiwa wananchi wa Arusha wamedhamiria kuonyesha dunia uungaji mkono wao kwa chama cha CDM.

Wednesday, October 3, 2012

BUS LA DAR EXPRESS LAWAKA MOTO NJIAPANDA YA TANGA (SEGERA)

Basi la  Dar Express limepata ajali ya kuungua moto jana asubuhi katika njia panda ya Dar, Arusha, Tanga (Segera) hakuna mtu aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha. Katika ajali hiyo mizigo yote iliteketea kwa moto huo ambapo abiria wengi waliokuwamo kwenye gari hilo walikuwa ni wanafuzi. lilitokea Rombo mkoani kilimanjaro.

Sunday, September 9, 2012

Sunday, June 10, 2012

Huduma mpya ya airtel jiunge Supa5 yawavutia wakazi wa iringa

Sehemu ya umati wa wakazi wa Iringa uliofurika jana kwenye uwanja wa Mwembe Togwa wakati wa utambulisho wa huduma mpya ya airtel Supa5 yenye lengo la kutoa huduma tano nafuu za huduma za mawasiliano kupitia Airtel.huduma hiyo itatambulishwa hivi karibuni katika mkoa wa Arusha na baadaye jijini Mwanza.Airtel Jiunge na Supa

Huduma mpya ya airtel jiunge Supa5 yawavutia wakazi wa iringa

 Mmoja wa Mwanamazingaombwe wa mjini Iringa aliyejitambulisha kwa jina la Almas a.k.a Afande Sele akionesha akadabla akadabla zake mbele ya umati wa wakazi wa Iringa waliojitokeza kwa wingi jana jioni kwenye uwanja wa Mwembe Togwa,mjini Iringa wakati wa utambulisho wa huduma mpya ya airtel Supa5 yenye lengo la kutoa huduma tano nafuu za huduma za mawasiliano kupitia Airtel.huduma hiyo itaendelea kutambulishwa tena katika mkoa wa Arusha na baadaye jijini Mwanza

Thursday, May 17, 2012

Hili ndilo Gari alilopatanalo ajali marehemu Patrick Mafisango maeneo ya TAZARA jijini Dar. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Simba bwana Aden Rage amesema kuwa taarifa za awali juu ya chanzo cha kifo cha mchezaji huyo zinasema kuwa mchezaji huyo amekutwa na mauti akiwa anaendesha gari na kujaribu kumkwepa mwendesha pikipiki.

Msiba huu unakuja wakati kocha wa timu ya Taifa ya Rwanda Milutin Sredovic 'Micho' akiwa amemteuwa kepteni wa zamani wa timu hiyo Hamada Ndikumana a.k.a 'Katauti' na Patrick Mafisango kujiunga na timu ya taifa hilo (AMAVUBI) kwaajili ya maandalizi ya nchi zitakazofuzu kwenda Brazil kwenye michuano ya Kombe la dunia 2014.

Kabla ya  kuichezea Simba mchezaji huyo alitokea Azam Fc ya jijini Dar es salaam.
Patrick Mafisango is dead.
Mwenyezi Mungu ilaze mahali pema peponi roho ya marehemu Patrick Mafisango.

Mchezaji Patrick Mafisango wa Simba afariki dunia

Mchezaji wa kimataifa Patrick Mafisango wa Simba SC
MCHEZAJI Patrick Mafisango wa timu ya Simba ya Dar es Salaam amefariki dunia leo kwa ajali ya gari katika eneo la Tazara jijini Dar es Salaam. Taarifa ambazo zimetolewa kutoka Klabu ya Simba zimesema Mafisango amefariki dunia leo asubuhi kwa ajali ya gari maeneo ya Tazara. Mtandao huu utawaletea taarifa zaidi za tukio hilo muda mfupi baadaye. Mtandao huu pia unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na klabu nzima ya Simba kwa pigo hilo.